Wednesday, July 10, 2013

MAFUNZO KUTOKA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

Wizara ya Maliasili na Utalii imewafunza wananchi

namna ya kubaini Asali isiyokuwa halisi ambayo

inadaiwa kutengezwa na wafanyabishara kwa

kutumia maji ya miwa yaliyochemshwa na

kubadilika kuwa sukari guru.

Akizungumza NIPASHE katika maonyesho ya

biashara ya 37 yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Jijini Dar e

Salaam jana, Ofisa nyuki na wakala wa huduma za misitu kutoka wizara hiyo,

Theresia Kamote, alisema kuna njia kadhaa za kuitambua asali iliyochakachuliwa.

Kamote alizitaja njia hizo kuwa ni pamoja na kuweka maji kwenye glasi na kisha

kumimina Asali na kwamba ikikaa chini ya glasi bila kuchanganyana na maji basi hiyo ni asilia na inakuwa haijachanganywa na chochote.

Alisema njia ya pili ni kuiweka Asali kwenye njiti ya kibiriti na kisha kuiwasha ikiwa

njiti hiyo itawaka basi Asali haijachakachuliwa kwa kuchanganywa na chochote lakini njiti ya kiberiti isipowaka inakuwa ni feki.

Aidha, Kamote aliongeza kuwa wizara yake imekuwa ikiwasisitiza wafanyabiashara

wa bidhaa hiyo kuwa waaminifu na kuwauzia wateja waoe bidhaa halisi na wale ambao bidhaa zao zinagundulika zimechakachuliwa ziharibiwa.

Aliongeza kuwa njia nyingine ni kuonja bidhaa hiyo na kwamba iliyokachuliwa kwa

kuchemsha inatoa harufu ya moshi tofauti na ambayo ni halisi.

“Wizara imekuwa ikitoa rai kwa wafanyabiashara wa bidhaa hiyo kuwa waaminifu na

pale tunapogundua bidhaa yenyewe ni feki sisi kama wizara huwa tunaiharibu,”

alisisitiza Kamote.

No comments:

Post a Comment