Wadau wote karibuni sana kwenye maonyesho ya wakulima ya nane nane na kupita kwenye banda la SUA ambapo mtajipatia asali safi na halisi toka HONEY SPRING.
Karibuni wote na mwambie na mwenzio aje apate mambo mazuri
This blog is devoted to give out different information concerning honey like different types of honey, their uses, how to differentiate real honey from fake ones and many other things. Come, educate yourself and place your order of good quality honey from honey spring.
Thursday, August 1, 2013
NANE NANE MOROGORO
Monday, July 22, 2013
ASALI NA KUTIBU MICHUBUKO AU VIDONDA
Asali imekua ikitumika katika kutibu michubuko au vidoka toka zamani na ilitumika zaidi katika kutibu vidonda vya wanajesgi katika vita vya dunia!
Asali ina tabia za "kianti-bacteria" kwasababu ya gesi ya HYROGEN PEROXIDE inayopatikana na hivyo kufanya iwe na uwezo wa kupambana na bacteria lakini pia kuzuia mazingira ya bacteria kuzaliana!
Kutokana na sababu hizo ni vyema kutokosa asali katika sehemu tunazokaa ili kuweza kua na uhakika wa kujiponya wenyewe kwa haraka zaidi bila kuhangaika!
Pichani anaonekana mtoto mwenye michubuko ikiwa imepakwa asali ambayo ilikausha michubuko hiyo baada ya siku chache
Wednesday, July 17, 2013
ASALI TOKA HONEY SPRING
Honey Spring tuna ujazo tofauti wa asali kuanzia lita 5 hadi 350ml tukilenga kufikia watu wote ili kuongeza matumizi ya asali katika jamii zetu.
ASALI YA NYUKI WAKUBWA ambayo kwetu sisi inaitwa WAKUBWA CLASSIC ina ujazo(ikiwa na bei kwenye mabano) wa LITA 5(60, 000), LITA 1(12, 000) na 350ml(5500)
ASALI YA NYUKI WADOGO ambayo kwetu sisi inaitwa WADOGO CLASSIC ina ujazo(ikiwa na bei kwenye mabano) wa LITA 5(175, 000), LITA 1(35, 000), NUSU LITA(20, 000) na 350ml(15, 000).
Ukiwa unahitaji asali toka kwetu na upo DAR ES SALAAM unaweza piga simu namba 0683370065 au 0769129351 na ukatoa order yako na ukaletewa asali ulipo.
Kwa wakazi wa MOROGORO karibuni sana katika duka pekee la asali mkoani morogoro lililopo katika ghorofa la LOTTOS.
Tuesday, July 16, 2013
HONEY
Not All Sugars are Equal
The reasoning here is not about eating excessively and a willful binging of sugary stuff, which is all straight-forward enough for us to leave that stone unturned. I am talking about choosing honey over other sugars and eating it for health. Knowledge such as "there are good calories and bad calories" and "not all fats are equal" all seem too common, especially amongst people who are dieting and weight conscious, however "all sugars are not created equal" sometimes seems to come across as counter intuitive and even bizarre. People need to know that there are good sugar, bad sugar and even dangerous sugar! And because there are so many guises of sweeteners, and some come in names that you can even pronounce, we must know how to read food labels critically!
Think about it. Which sugar amongst all sugars fits this behavior - it is anabolic, medicinal, antiseptic, anti-cancer, gentle on blood sugar, friendliest to our liver, the most ideal fuel for burning body fats, and has many healing effects? None, except honey. Taste aside (though I vote it as the tastiest sugar, sweetest medicine), I believe bee's sugar is the best, nature-given sugar for our body, yet probably most forgotten and neglected sweetener. The doctors never fail to tell us that our body is unable to utilize refined sugars which are void of all nutrients and our body tissues in fact must relinquish precious vitamins and minerals to detoxify and eliminate them from our system, which often leads to nutrient deficiencies and the gradual deterioration of our cells and organs. But did they ever tell you once that our body needs some sugar, and good sugar, honey ideally, can provide a positive supply of liver glycogen for healthy effects of brain metabolism?
Friday, July 12, 2013
FAIDA ZA ASALI
Sukari iliyoko kwenye asali humengenyuka kwa urahisi sana, na kugeuka kuwa glukosi na fruktosi kwa haraka. Hata kwa wale wenye matumbo mabovu (yenye maradhi).
Asali husaidia pia figo na utumbo kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa.
Asali ina kalories chache sana, ukilinganisha na kiwango cha sukari kilichomo kwenye asali, cha ajabu ni kuwa hutoa nishati (energy) nyingi katika mwili, lakini haisababishi ongezeko la mwili yaani unene. (Cholesterol)
Asali huyeyuka kwa haraka sana kuingia kwenye damu, ukilinganisha na vinywaji vingine, kama maji ya kawaida. Asali huchukua takriban dakika saba tu kuingia katika mfumo wa damu.
Asali husaidia hutengenezaji wa damu mwilini, kwani hutoa nishati au nguvu inayosababisha hutengenezaji wa damu kuwa rahisi. Vilevile asali usafisha damu, katika mzunguko wake, na kusaidia mzunguko wa damu kuwa rahisi na mwepesi. Asali husadia kulinda mishipa ya damu isiathirike na maradhi yanayoshambulia mishipa ya damu. Asali pia husaidia kulinda ubongo na kuuwezesha kufanya kazi vizuri na upesi zaidi. Asali husaidia kuua bakteria wa aina mbalimbali inapotumiwa kwa matibabu na hasa kwenye vidonda. Pia asali husaidia kuondoa matatizo ya tishu (Tisue Difficiency) na udhaifu kwenye mwili (Body Frailty).
MANUFAA YA ASALI
Zaidi ya kuwa tu chakula kinachofaa, asali ni mojawapo ya dawa za zamani zaidi zinazotumika, kwani ina vitamini B nyingi, madini kadhaa, na vitu vyenye uwezo wa kuzuia utendaji wa oksijeni. Dakt. May Berenbaum, mtaalamu wa wadudu katika Chuo Kikuu cha Illinois, Marekani, anasema: “Asali imetumiwa kwa karne nyingi kutibu matatizo mengi ya afya kama vile vidonda, kuungua, watoto wa jicho, vidonda vya ngozi na majeraha ya kukwaruzwa.”
Likieleza kuhusu upendezi wa hivi karibuni kuhusu manufaa za asali kwa afya, Shirika la Habari la CNN linaripoti hivi: “Asali iliacha kupakwa kwenye vidonda wakati dawa za kuua viini vya ugonjwa zilipovumbuliwa wakati wa Vita vya Pili vya Ulimwengu. Lakini utafiti mpya na kutokea kwa bakteria zisizoweza kuuawa na dawa hizo umefanya asali ianze kutumiwa tena.” Kwa mfano, sehemu moja ya utafiti huo inahusu kutibu majeraha ya kuungua. Ilionekana kwamba wagonjwa walipona haraka na kuhisi maumivu machache na kuwa na makovu machache walipotibiwa kwa asali.
Uchunguzi unaonyesha kwamba kwa sababu ya kimeng’enya fulani kinachoongezwa kwenye nekta na nyuki, asali ina uwezo wa kupigana na bakteria na viini. Kimeng’enya hicho hutokeza haidrojeni peroksaidi, ambayo huua bakteria hatari. Isitoshe, inapopakwa juu ya kidonda, asali hupunguza mwasho na kuchochea ukuzi wa tishu zinazofaa. Hivyo, mtaalamu wa biolojia na kemia Dakt. Peter Molan wa New Zealand anasema: “Wataalamu wa matibabu wanaiona asali kuwa dawa nzuri, inayofaa kwa matibabu.” Kwa kweli, Shirika la Matibabu la Australia limeidhinisha asali kuwa dawa, na asali huuzwa kama dawa ya kutibu vidonda katika nchi hiyo.
Ni vyakula gani vingine vitamu ambavyo hujenga mwili na vinavyoweza kutumiwa kama dawa? Si ajabu kwamba zamani sheria zilipitishwa ili kulinda nyuki na wafugaji wa nyuki! Ilikuwa kosa kukata miti au kuharibu mizinga yenye nyuki, na mtu angeweza kuadhibiwa kwa kutozwa faini kubwa au hata kuuawa
Thursday, July 11, 2013
ASALI NI NINI?
Sasa basi Asali ni nini? Asali ni mchanganyiko wa virutubisho mbali mbali, zikiwemo aina ya sukari zinazojulikana kwa jina la Glukosi (Glucose) pamoja na Fruktosi (Fructose), na madini mbalimbali vikiwemo; Magnesium, Copper, Iodine, zinc, Potassium, Calcium, Sodium, Chlorine, Sulfur, Iron na Phosphate, pamoja na vitamin B1, B2, B3, B5, B6, na vitamin C. Vitamin mara nyingi ubadilika kulingana na ubora wa necta, pamoja na chavua. Vile vile kwenye asali, kunapatikana aina mbalimbali za Hormones. Kama inavyoelezwa kuwa asali ni ponyo(kinywaji chenye kutibu) kwa wanadamu, na haya yamethibiti kwa wanadamu hivi leo. Kama ilivyotokea katika mkutano wa wanasayansi, uliofanyika mwaka 1993 mwezi Sept. tarehe 20-26. Mkutano huu ulifanyika nchini China, na ulijulikana kwa jina la World Apiculture Comference. Na kuchapishwa katika jarida la Horriget News Paper, la tarehe 19th.Oct.1993. Katika mkutano huo matibabu ya kutumia asali yalijadiliwa kwa mapana sana, wanasayansi wa Kimarekani wao walielezea kuwa, ndani ya asali kuna vitu vinaitwa; Royal Jelly, chavua, na ute (Propolis, Bee resin), vitu hivi husaidia sana katika matibabu ya magonjwa mengi. Naye Daktari kutoka Romania, yeye aliwahi kujaribu kutibu mtoto wa jicho (Cataract), kwa wagonjwa 2094, kati yao 2002 walipona kabisa, na hii ni sawa na asilimia 96% ya wagonjwa waliopona kabisa. Daktari huyo alieleza kuwa Bee Resin au ute unaotokana na nyuki, unasaidia kuponyesha magonjwa mengine, mfano magonjwa ya ngozi (Skin Diseases), magonjwa ya kuvuja kwa damu (Haemorrhoid), magonjwa ya uzazi (Gynaecological Diseases) n.k.
HONEY AND BURNS
This is why it is recommended to have at least a small amount of honey at any time in our homes because accidents occur without warning!
Follow the instructions on the picture and you will be oky.
Wednesday, July 10, 2013
STINGLESS BEES HONEY vs STINGING BEES HONEY
How can I tell the difference between honey bee honey and stingless bee honey?
Stingless bee honey is more liquid than the well known honey bee honey. Honey bee honey has a water content of about 20% while the stingless bees has a water content of between 20-42%, depending on the species and the area from where the honey is collected. The high water content in stingless bee honey makes it very prone to fermentation. The flavor is often described as a more flowery than honey bee honey, but it depends largely on the species. There has been relatively little scientific research into the medical properties attributed to honey from stingless bees, but due to the presumption that it is a remedy and the usually low amount of honey produced, the price is much higher than that of honey bee honey (Apis mellifera).
IJUE ASALI ZAIDI
VIRUTUBISHO VILIVYOPO NDANI YA ASALI
Asali ina virutubisho lukuki vinavyoifanya iwe ni chakula bora na dawa madhubuti ya kutibu magonjwa mengi. Kutokana na kuwa na kiasi kikubwa sana cha sukari. (high sugar concentration) kikaribiacho 80%( huku 20% iliyobaki ni maji) huifanya asali iwe na tabia ya kuua vimelea (antibiotic properties) na kuzuia vimelea kuzaliana na kukua. Asali pia ina vimeng'enyo ( enzymes) ambavyo hutengeneza kemikali iitwayo Hydrogen peroxide (H202) , kemikali hii ina uwezo wa kuua bacteria wengi kwa wigo mkubwa (kills bacteria in abroad spectrum) na pia asali ina tindikali nyingi (highly acidic) kuiwezesha pia kuua vimelea. Asali ina vitamini na madini mbali mbali yanayoifanya iwe ni moja ya vyakula bora Duniani.
Source FANO 2010 products
MAFUNZO KUTOKA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
Wizara ya Maliasili na Utalii imewafunza wananchi
namna ya kubaini Asali isiyokuwa halisi ambayo
inadaiwa kutengezwa na wafanyabishara kwa
kutumia maji ya miwa yaliyochemshwa na
kubadilika kuwa sukari guru.
Akizungumza NIPASHE katika maonyesho ya
biashara ya 37 yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Jijini Dar e
Salaam jana, Ofisa nyuki na wakala wa huduma za misitu kutoka wizara hiyo,
Theresia Kamote, alisema kuna njia kadhaa za kuitambua asali iliyochakachuliwa.
Kamote alizitaja njia hizo kuwa ni pamoja na kuweka maji kwenye glasi na kisha
kumimina Asali na kwamba ikikaa chini ya glasi bila kuchanganyana na maji basi hiyo ni asilia na inakuwa haijachanganywa na chochote.
Alisema njia ya pili ni kuiweka Asali kwenye njiti ya kibiriti na kisha kuiwasha ikiwa
njiti hiyo itawaka basi Asali haijachakachuliwa kwa kuchanganywa na chochote lakini njiti ya kiberiti isipowaka inakuwa ni feki.
Aidha, Kamote aliongeza kuwa wizara yake imekuwa ikiwasisitiza wafanyabiashara
wa bidhaa hiyo kuwa waaminifu na kuwauzia wateja waoe bidhaa halisi na wale ambao bidhaa zao zinagundulika zimechakachuliwa ziharibiwa.
Aliongeza kuwa njia nyingine ni kuonja bidhaa hiyo na kwamba iliyokachuliwa kwa
kuchemsha inatoa harufu ya moshi tofauti na ambayo ni halisi.
“Wizara imekuwa ikitoa rai kwa wafanyabiashara wa bidhaa hiyo kuwa waaminifu na
pale tunapogundua bidhaa yenyewe ni feki sisi kama wizara huwa tunaiharibu,”
alisisitiza Kamote.
Friday, July 5, 2013
KUOKA KWA KUTUMIA ASALI
Kwenye picha ni vitu vya kuzingatia ukiwa unatumia ASALI badala ya sukari katika kuoka vitu mbalimbali!
Tuanze kutumia asali sasa
ASALI na MDALASINI
Mchanganyiko huu ni tiba kubwa sana ambayo imekua ikishauriwa na matabibu kote duniani na bado tafiti mbali mbali zinaendelea kufanyika kuhusu mchanganyiko huu!
Tusiache afya zetu zidorore wakati dawa tunazo majumbani
Wednesday, July 3, 2013
MAJI KWENYE ASALI
Katika vitu ambavyo ni changamoto kubwa sana katika soko la asali na vinawasumbua si tu watumiaji wa asali bali hata wa wauzaji ni kiwango kikubwa cha maji katika asali kuliko kawaida ambacho chanzo huweza kua UWAHISHAJI WA KUVUNA ASALI KABLA HAIJAKOMAA VIZURI au tatizo kubwa zaidi ambalo ni UCHAKACHUAJI WA ASALI KWA KUONGEZA MAJI unaofanywa na wauzaji wasio waaminifu.
Kwa kawaida ASALI YA NYUKI WAKUBWA inakua na kiwango cha maji ya kati ya asilimia 17 mpaka 20 na asilimia inayobaki ni SUKARI. Wakati asali ya nyuki wadogo kiwango cha maji kinakua zaidi ya asilimia 20.
MAJI ni adui mkubwa sana katika asali kwani maji yakizidi hupunguza ubora wa asali, lakini pia huiweka asali katika hatari kubwa ya kuchacha.
Zipo njia nyingi za kienyeji za kupima kiwango cha maji kwenye asali na kujua kama maji yaliyopo ni ya kiwango sahihi ama la! Njia hizo ni pamoja na kutumia MSHUMAA, KARATASI NYEUPE, KUDONDOSHEA ASALI KWENYE KIKOMBE CHA MAJI n.k.
Pamoja na uwepo wa njia hizo lakini honey spring tumekwenda hatua moja mbele na tunatumia kifaa kidogo cha mkononi kinachoitwa REFRACTOMETER ambacho hupima kwa usahihi zaidi kiwango cha MAJI na SUKARI pia katika asali.
Kifaa hichi kinatuwezesha kuingiza sokoni asali ambayo inatakiwa kupelekwa kwa mlaji lakini pia kwa kiwango ambacho mlaji anakitegemea kwenye asali anayonunua!
Kwenye maonyesho ya nane nane(88) mwaka huu mkoani MOROGORO tutakuepo na kuonyesha vizuri zaidi watumiaji jinsi kifaa hichi kinavyofanya kazi.
Tuesday, July 2, 2013
ASALI NA RANGI ZAKE
Asali duniani kote haina rangi moja maalumu, ni muhimu sana kujua hilo!
Asali hutofautiana rangi kutokana na aina ya maua ambayo nyuki wanachukua nectar zao lakini pia kutokana na asali imekaa mda gano toka ilipovunwa na kuhifadhiwa!
Hautakiwi kustuka unapokutana na rangi tofauti ya asali kuliko ile uliyoizoea, mfano wa rangi za asali ni kama zinavyoonekana asali za rangi tofauti tofauti kwenyw picha!!
VITU VYA MOTO HAPANA
nawakaumbusha mnapotumia ASALI usiweke kwenye maji ya moto au chai ya moto sana kwasababu kwa kufanya hvyo utaua enzymes(vimeng'enyo) vyenye manufaa katika mwili!!
Asali ichanganywe kwenye maji au chai ya uvuguvugu ili kutoharibu uhalisia wake!!
MCHANGANYIKO WA ASALI NA MDALASNI
Asubuhi njema
Monday, July 1, 2013
KUTAMBUA ASALI HALISI
Kutokana na udanganyifu ambao watu wamekua wakifanya kwa kuchanganya asali na maji, sukari na vitu vingine ambavyo sio asali ni muhimu kujua njia za kutambua uhakisia wa asali!!
Njia mojawapo ni ya kutumia MSHUMAA katika kutambua uhalisia wa asali!
Chukua mshumaa na kisha chovya utambi wake katika asali kisha washa moto utambi. Endapo utambi utawaka basi asali hiyo ni halisi kwa maana ikiwa imechanganywa na kitu ambacho sio asali utambi hautaweza kuwaka.
Fata step kama inavyoonekana kwenye picha.
Sunday, June 30, 2013
UTATOFAUTISHAJE ASALI YA NYUKI WAKUBWA NA WADOGO?
Njia rahisi kabisa ya kutofautisha ni kwa kuonja asali hizo kwani zina LADHA tofauti.
ASALI YA NYUKI wadogo ina ladha ya UCHACHU inapomalizikia mdomoni wakati
ASALI YA NYUKI WAKUBWA yenyewe in a ladha ya UTAMU moja kwa moja bila kuacha uchachu mdomoni.
Njia nyingine ya kutofautisha kati ya asali hizi ni kua ASALI YA NYUKI WADOGO ni nyepesi zaidi kwasababu ina kiwango kikubwa zaidi cha maji kuliko ASALI YA NYUKI WAKUBWA ambayo ina kiwango kidogo cha maji na hivyo kuifanya iwe nzito zaidi.
TAHADHARI: Asali tunazozungumzia hapa ni zile ambazo ni HALISI na sio zilizochakachuliwa kwa njia yoyote.
AINA MBILI ZA ASALI NI...
Kuna aina kuu mbili za ASALI ambazo ndizo zinazojulikana ulimwenguni kote!
Aina hizo ni ASALI YA NYUKI WADOGO ( au asali ya nyuki wasiouma) na ASALI YA NYUKI WAKUBWA ( au asali ya nyuki wanaouma).
Aina hizo kuu mbili za nyuki ndizo zinatoa aina mbili kuu za asali!
Hivyo jambo la muhimu kujua kabla ya kununua asali ni kua kuna aina mbili za asali na hivyo ni lazma ujue unahitaji asali ipi, eidha ya NYUKI WAKUBWA au NYUKI WADOGO!
Ntakuja kueleza utofauti uliopo na jinsi gani ya kugundua utofauti uliopo kati ya aina hizo mbili za asali!
Usiache kufuatilia..
Picha inamuonyesha kushoto nyuki mkubwa anaeuma na kulia nyuki mdogo asieuma.