Kama tujuavyo kua kuna aina mbili za asali ambazo ni ASALI YA NYUKI WAKUBWA na ASALI YA NYUKI WADOGO. Swali ni je mtu utatofautishaje kwa urahisi asali hizi na kuepuka kuibiwa na wajanja kabla ya kununua!!
Njia rahisi kabisa ya kutofautisha ni kwa kuonja asali hizo kwani zina LADHA tofauti.
ASALI YA NYUKI wadogo ina ladha ya UCHACHU inapomalizikia mdomoni wakati
ASALI YA NYUKI WAKUBWA yenyewe in a ladha ya UTAMU moja kwa moja bila kuacha uchachu mdomoni.
Njia nyingine ya kutofautisha kati ya asali hizi ni kua ASALI YA NYUKI WADOGO ni nyepesi zaidi kwasababu ina kiwango kikubwa zaidi cha maji kuliko ASALI YA NYUKI WAKUBWA ambayo ina kiwango kidogo cha maji na hivyo kuifanya iwe nzito zaidi.
TAHADHARI: Asali tunazozungumzia hapa ni zile ambazo ni HALISI na sio zilizochakachuliwa kwa njia yoyote.
I like.
ReplyDeletethanks Beatrice and welcome to become a member of our blog
Delete