Thursday, July 11, 2013

HONEY AND BURNS

This is why it is recommended to have at least a small amount of honey at any time in our homes because accidents occur without warning!

Follow the instructions on the picture and you will be oky.

Wednesday, July 10, 2013

STINGLESS BEES HONEY vs STINGING BEES HONEY

How can I tell the difference between honey bee honey and stingless bee honey?

Stingless bee honey is more liquid than the well known honey bee honey. Honey bee honey has a water content of about 20% while the stingless bees has a water content of between 20-42%, depending on the species and the area from where the honey is collected. The high water content in stingless bee honey makes it very prone to fermentation. The flavor is often described as a more flowery than honey bee honey, but it depends largely on the species. There has been relatively little scientific research into the medical properties attributed to honey from stingless bees, but due to the presumption that it is a remedy and the usually low amount of honey produced, the price is much higher than that of honey bee honey (Apis mellifera).

IJUE ASALI ZAIDI

VIRUTUBISHO VILIVYOPO NDANI YA ASALI

Asali ina virutubisho lukuki vinavyoifanya iwe ni chakula bora na dawa madhubuti ya kutibu magonjwa mengi. Kutokana na kuwa na kiasi kikubwa sana cha sukari. (high sugar concentration) kikaribiacho 80%( huku 20% iliyobaki ni maji)  huifanya asali iwe na tabia ya kuua vimelea (antibiotic properties) na kuzuia vimelea kuzaliana na kukua. Asali pia ina vimeng'enyo ( enzymes) ambavyo hutengeneza kemikali iitwayo Hydrogen peroxide (H202) , kemikali hii ina uwezo wa kuua bacteria wengi kwa wigo mkubwa (kills bacteria in abroad spectrum) na pia asali ina tindikali nyingi (highly acidic) kuiwezesha pia kuua vimelea. Asali ina vitamini na madini mbali mbali yanayoifanya iwe ni moja ya vyakula bora Duniani.

Source FANO 2010 products

MAFUNZO KUTOKA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

Wizara ya Maliasili na Utalii imewafunza wananchi

namna ya kubaini Asali isiyokuwa halisi ambayo

inadaiwa kutengezwa na wafanyabishara kwa

kutumia maji ya miwa yaliyochemshwa na

kubadilika kuwa sukari guru.

Akizungumza NIPASHE katika maonyesho ya

biashara ya 37 yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere Jijini Dar e

Salaam jana, Ofisa nyuki na wakala wa huduma za misitu kutoka wizara hiyo,

Theresia Kamote, alisema kuna njia kadhaa za kuitambua asali iliyochakachuliwa.

Kamote alizitaja njia hizo kuwa ni pamoja na kuweka maji kwenye glasi na kisha

kumimina Asali na kwamba ikikaa chini ya glasi bila kuchanganyana na maji basi hiyo ni asilia na inakuwa haijachanganywa na chochote.

Alisema njia ya pili ni kuiweka Asali kwenye njiti ya kibiriti na kisha kuiwasha ikiwa

njiti hiyo itawaka basi Asali haijachakachuliwa kwa kuchanganywa na chochote lakini njiti ya kiberiti isipowaka inakuwa ni feki.

Aidha, Kamote aliongeza kuwa wizara yake imekuwa ikiwasisitiza wafanyabiashara

wa bidhaa hiyo kuwa waaminifu na kuwauzia wateja waoe bidhaa halisi na wale ambao bidhaa zao zinagundulika zimechakachuliwa ziharibiwa.

Aliongeza kuwa njia nyingine ni kuonja bidhaa hiyo na kwamba iliyokachuliwa kwa

kuchemsha inatoa harufu ya moshi tofauti na ambayo ni halisi.

“Wizara imekuwa ikitoa rai kwa wafanyabiashara wa bidhaa hiyo kuwa waaminifu na

pale tunapogundua bidhaa yenyewe ni feki sisi kama wizara huwa tunaiharibu,”

alisisitiza Kamote.

Friday, July 5, 2013

KUOKA KWA KUTUMIA ASALI

Kwenye picha ni vitu vya kuzingatia ukiwa unatumia ASALI badala ya sukari katika kuoka vitu mbalimbali!
Tuanze kutumia asali sasa

ASALI na MDALASINI

Mchanganyiko huu ni tiba kubwa sana ambayo imekua ikishauriwa na matabibu kote duniani na bado tafiti mbali mbali zinaendelea kufanyika kuhusu mchanganyiko huu!
Tusiache afya zetu zidorore wakati dawa tunazo majumbani

Wednesday, July 3, 2013

MAJI KWENYE ASALI

Katika vitu ambavyo ni changamoto kubwa sana katika soko la asali na vinawasumbua si tu watumiaji wa asali bali hata wa wauzaji ni kiwango kikubwa cha maji katika asali kuliko kawaida ambacho chanzo huweza kua UWAHISHAJI WA KUVUNA ASALI KABLA HAIJAKOMAA VIZURI au tatizo kubwa zaidi ambalo ni UCHAKACHUAJI WA ASALI KWA KUONGEZA MAJI unaofanywa na wauzaji wasio waaminifu.

Kwa kawaida ASALI YA NYUKI WAKUBWA inakua na kiwango cha maji ya kati ya asilimia 17 mpaka 20 na asilimia inayobaki ni SUKARI. Wakati asali ya nyuki wadogo kiwango cha maji kinakua zaidi ya asilimia 20.

MAJI ni adui mkubwa sana katika asali kwani maji yakizidi hupunguza ubora wa asali, lakini pia huiweka asali katika hatari kubwa ya kuchacha.

Zipo njia nyingi za kienyeji za kupima kiwango cha maji kwenye asali na kujua kama maji yaliyopo ni ya kiwango sahihi ama la! Njia hizo ni pamoja na kutumia MSHUMAA, KARATASI NYEUPE, KUDONDOSHEA ASALI KWENYE KIKOMBE CHA MAJI n.k.

Pamoja na uwepo wa njia hizo lakini honey spring tumekwenda hatua moja mbele na tunatumia kifaa kidogo cha mkononi kinachoitwa REFRACTOMETER ambacho hupima kwa usahihi zaidi kiwango cha MAJI na SUKARI pia katika asali.

Kifaa hichi kinatuwezesha kuingiza sokoni asali ambayo inatakiwa kupelekwa kwa mlaji lakini pia kwa kiwango ambacho mlaji anakitegemea kwenye asali anayonunua!

Kwenye maonyesho ya nane nane(88) mwaka huu mkoani MOROGORO tutakuepo na kuonyesha vizuri zaidi watumiaji jinsi kifaa hichi kinavyofanya kazi.